• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Complaints |
    • Gms |
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

  • Mwanzo
  • About KMC
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa taasisi
    • Core Functions
  • Utawala
    • Idara
      • Human Resources and Administration
      • Health and Sanitation
      • Finance
      • Planning and Commercial
    • Vitengo
      • Maintenance Service
      • Internal Audit
      • Procurement Management
      • Information and Communication Technologies
      • Legal Services
      • Security
  • Kituo cha habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya picha
    • Press-Releases
    • Video
  • Marketing
    • Products and Services
    • Marketing Price
  • Investment and Projects
    • Ongoing Projects
    • Miradi iliyokamilika
    • Upcoming Projects
    • Fursa za Uwekezaji
  • Manunuzi
    • Tenders
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Journals/Newsletter
    • Reports
    • Hotuba
  • E- Services Links
    • Revenue Collection(TAUSI)
    • GISP Portal
    • Employees Self Service Portal
    • E - Mrejesho
    • E - Board
    • E - Mikutano

Dkt. Jafo: Wafanyabiashara Kariakoo Kuweni Mabalozi wa Amani

Posted on: August 15th, 2025

Wafanyabiashara wa Soko la Kariakoo wametakiwa kuwa mabalozi wa kuhakikisha nchi inaendelea kuwa na amani kipindi chote cha kuelekea Uchaguzi Mkuu ili shughuli za biashara zifanyike kwa usalama huku wakilipa kodi kwa uaminifu.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Selemani Jafo wakati wa hotuba yake ya ufunguzi wa tamasha la Gulio la Kariakoo (Kariakoo Festival) leo (15 Agosti 2025) Dar es Salaam lenye lengo la kutangaza fursa za biashara na masoko yaliyopo nchini.

“Tarehe 29 Oktoba mwaka huu tutakuwa na Uchaguzi Mkuu, niwaalike wafanyabiashara wa Kariakoo kuwa mabalozi wa amani ili shughuli za kibiashara katika eneo lote la Kariakoo na Tanzania kwa ujumla zifanyike kwa amani na utulivu” alisisitiza Dkt. Jafo.

Naye Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) Yusuph Mwenda alisisitiza kuwa iko tayari kuendelea kuwasikiliza wafanyabiashara na kutatua kero zao ili walipe kodi kwa mujibu wa Sheria.

Mwenda aliongeza kuwataka wafanyabiashara kote nchini kuendelea kulipa kodi kwa uaminifu ili Serikali ipate mapato ya kutekeleza miradi ya maendeleo.

Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo CPA Ashraph Abdulkarim alieleza kuwa tamasha hilo ni fursa nzuri kwa wadau wa Soko la Kariakoo kuwafikia wateja ndani na nje ya nchi.

CPA Abdulkarim aliongeza kusema, Shirika lipo kwenye maandalizi ya mwisho kuelekea kurejesha wafanyabiashara ndani ya Soko baada ya Serikali kukamilisha ujenzi na ukarabati wa soko ambapo amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha Bilioni 28.

Mwisho.

Matangazo

  • Taarifa kwa Umma January 31, 2025
  • Taarifa kwa Umma January 29, 2025
  • Usajili wa wafanyabiashara November 14, 2023
  • Tangazo la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 August 15, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Maandalizi Ufunguzi wa Soko la Kariakoo Yakamilika

    October 11, 2025
  • Meneja Mkuu Shirika la Masoko Kariakoo, Bw. Ashiraf Abdulkarim anasema Kariakooo ndiyo Soko kubwa ambalo wafanyabiashara wa ndani na nje ya mipaka ya Tanzania wanakuja kufanya biashara.

    September 24, 2025
  • Dkt. Jafo: Wafanyabiashara Kariakoo Kuweni Mabalozi wa Amani

    August 15, 2025
  • Soko la Kariakoo Kuwa na Bima ya Majanga

    July 31, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TAMISEMI
  • eGovernment Authority
  • Employees Self Service Portal

Viunganishi Linganifu

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    General Manager, Kariakoo Markets Corporation, Nyamwezi/Tandamti Street,

    Anuani ya posta: P. O. Box 15789 Dar es Salaam, Tanzania

    Simu: +255 22 2180678

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe za Watumishi: info@kariakoomarket.co.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

www.freevisitorcounters.com

    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2024 Shirika la Masoko ya Kariakoo . All rights reserved.