• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Complaints |
    • Gms |
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
    • Majukumu ya msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Human Resources and Administration
      • Health and Sanitation
      • Finance
      • Planning and Commercial
    • Vitengo
      • Maintenance Service
      • Internal Audit
      • Procurement Management
      • Information and Communication Technologies
      • Legal Services
      • Security
  • Kituo cha habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya picha
    • Press-Releases
    • Video
  • Marketing
    • Products and Services
    • Marketing Price
  • Miradi na Fursa za uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Manunuzi
    • Zabuni
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Journals/Newsletter
    • Reports
    • Hotuba
  • Huduma mtandao
    • Revenue Collection(TAUSI)
    • GISP Portal
    • Employees Self Service Portal
    • E - Mrejesho
    • E - Board
    • E - Mikutano

KARIAKOO KUSAJILI TAARIFA ZA WAFANYA BIASHARA WAKE KATIKA KANZI DATA MAALUM

Posted on: January 11th, 2026

KARIAKOO KUSAJILI TAARIFA ZA WAFANYA BIASHARA WAKE KATIKA KANZI DATA MAALUM

Shirika la Masoko ya Kariakoo limekamilisha maandalizi ya kuanzisha kanzi data maalum ya wafanyabiashara wa soko la Kariakoo, kanzi data ambayo itakuwa na taarifa kamili ya mfanyabiashara ikionesha majina kamili, aina ya biashara, namba ya eneo la biashara, ukubwa wa eneo namba ya mlipakodi na namba ya kitambulisho cha taifa, malipo anayostahili kulipa pamoja na kiasi kilicholipwa.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo CPA.Ashraph Abdulkarim, kuandaliwa kwa kazi data hiyo kunatokana na maboresho ya mifumo ya tehama ambayo inawezesha soko hilo kutunza taarifa zake kwa njia ya kidigitali jambo ambalo ni muhimu katika kuzuia upotevu wa nyaraka na taarifa.

“Kanzi data hii italiwezesha shirika kupata taarifa sahihi za wafanyabiashara wake kwa wakati ambapo taarifa hizi huishi kwa muda mrefu na pia haziwezi kuathiriwa na changamoto ya mvua au kuharibika kwa namna yeyote ile” amebainisha CPA. Ashraph Abdulkarim

CPA. Abdulkarim ameongeza kuwa uwepo wa kanzi data hiyo ni mwendelezo wa mikakati ya shirika hilo kuendelea kusimamia ukusanyaji na udhibiti wa mapato ya shirika hilo ili soko la Kariakoo liendelee kuzalisha kwa tija na uwekezaji uliofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kukarabati na Kujenga upya soko hilo la Kimataifa hapa nchini.

Ikumbukwe kuwa Soko la Kariakoo liliungua mwaka 2021, ambapo serikali ilianza ukarabati na ujenzi wa soko hilo upya mwaka 2022 ambapo mpaka sasa ukarabati na ujenzi huo umekamilika kwa asilimia 99 na soko hilo litafunguliwa hivi karibuni.

Matangazo

  • Taarifa kwa Umma January 31, 2025
  • Taarifa kwa Umma January 29, 2025
  • Usajili wa wafanyabiashara November 14, 2023
  • Tangazo la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 August 15, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KARIAKOO KUSAJILI TAARIFA ZA WAFANYA BIASHARA WAKE KATIKA KANZI DATA MAALUM

    January 11, 2026
  • SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO, SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI JESHI LA POLISI WAKUTANA KUJADILI MIKAKATI YA ULINZI SOKO LA KARIAKOO.

    January 09, 2026
  • WATUMISHI WA WASHIRIKA LA MASOKO WAJENGEWA UWEZO MATUMIZI YA E-MREJESHO.

    January 08, 2026
  • SOKO LA KARIAKOO LATENGA VYUMBA MAALUM VYAA KUNYONYESHA KWA WAKINA MAMA.

    December 30, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TAMISEMI
  • eGovernment Authority
  • Employees Self Service Portal

Viunganishi Linganifu

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

Visitors Counter

www.freevisitorcounters.com

    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2024 Shirika la Masoko ya Kariakoo . All rights reserved.