• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Complaints |
    • Gms |
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

  • Mwanzo
  • About KMC
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa taasisi
    • Core Functions
  • Utawala
    • Idara
      • Human Resources and Administration
      • Health and Sanitation
      • Finance
      • Planning and Commercial
    • Vitengo
      • Maintenance Service
      • Internal Audit
      • Procurement Management
      • Information and Communication Technologies
      • Legal Services
      • Security
  • Kituo cha habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya picha
    • Press-Releases
    • Video
  • Marketing
    • Products and Services
    • Marketing Price
  • Investment and Projects
    • Ongoing Projects
    • Miradi iliyokamilika
    • Upcoming Projects
    • Fursa za Uwekezaji
  • Manunuzi
    • Tenders
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Journals/Newsletter
    • Reports
    • Hotuba
  • E- Services Links
    • Revenue Collection(TAUSI)
    • GISP Portal
    • Employees Self Service Portal
    • E - Mrejesho
    • E - Board
    • E - Mikutano

Soko la Kariakoo Kuwa na Bima ya Majanga

Posted on: July 31st, 2025

Shirika la Masoko ya Kariakoo limesaini mkataba wa makubaliano na Shirika la Bima la Taifa kwa ajili ya menejimenti ya vihatarishi vitakavyoweza kutokea katika soko jipya la Kariakoo hatua itakayosaidia kupata fidia ya hasara.


Mkataba huo wa makubaliano ya utoaji huduma za bima kwa Soko jipya la Kariakoo umesainiwa baina ya Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo CPA Ashraph Abdulkarim na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa Kaimu Abdi Mkeyenge leo (Jumatano (30 Julai 2025) jijini Dar es Salaam.


Akieleza lengo la mkataba huo CPA Abdulkarim alisema Serikali ya Awamu ya Sita imewekeza zaidi ya shilingi Bilioni 28 kujenga na kukarabati soko baada ya ajali ya moto ya 10 Julai 2021 hivyo ni budi kulinda miundombinu hiyo kwa kukata bima.


CPA Abdulkarim aliongeza kusema uamuzi huo umelenga kulinda mali za umma na kwamba wafanyabiashara watakaoingia ndani ya soko jipya la Kariakoo pia wataelimishwa kupata huduma za bima ili kukinga na majanga.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa Kaimu Abdi Mkenyenge alisema Shirika hilo ni kampuni ya Serikali yenye jukumu la kutoa huduma bora za bima hivyo uamuzi wa Soko la Kariakoo kuwa na bima umekuja wakati sahihi.


Mkeyenge aliongeza kusema, Shirika lake litatoa huduma bora za bima kwa Taasisi zote za umma na binafsi ili majanga yakitokea waweze kurudishiwa hasara itakayokuwa imetokea.


Mkurugenzi huyo alitoa wito kwa taasisi zingine zilizopo chini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI ikiwemo halmashauri nchini zenye majengo ya masoko kupata huduma za bima ili kuepusha hasara pale matukio ya vihatarishi ikiwemo moto yatakapotokea.


Shirika la Masoko ya Kariakoo lipo kwenye maandalizi ya ufunguzi wa soko baada ya kukamilika kwa mradi wa ujenzi na ukarabati ambapo wafanyabiashara watarejeshwa kuendelea na biashara.


Mwisho


Matangazo

  • Taarifa kwa Umma January 31, 2025
  • Taarifa kwa Umma January 29, 2025
  • Usajili wa wafanyabiashara November 14, 2023
  • Tangazo la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 August 15, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Maandalizi Ufunguzi wa Soko la Kariakoo Yakamilika

    October 11, 2025
  • Meneja Mkuu Shirika la Masoko Kariakoo, Bw. Ashiraf Abdulkarim anasema Kariakooo ndiyo Soko kubwa ambalo wafanyabiashara wa ndani na nje ya mipaka ya Tanzania wanakuja kufanya biashara.

    September 24, 2025
  • Dkt. Jafo: Wafanyabiashara Kariakoo Kuweni Mabalozi wa Amani

    August 15, 2025
  • Soko la Kariakoo Kuwa na Bima ya Majanga

    July 31, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TAMISEMI
  • eGovernment Authority
  • Employees Self Service Portal

Viunganishi Linganifu

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    General Manager, Kariakoo Markets Corporation, Nyamwezi/Tandamti Street,

    Anuani ya posta: P. O. Box 15789 Dar es Salaam, Tanzania

    Simu: +255 22 2180678

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe za Watumishi: info@kariakoomarket.co.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

www.freevisitorcounters.com

    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2024 Shirika la Masoko ya Kariakoo . All rights reserved.