• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Complaints |
    • Gms |
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

  • Mwanzo
  • About KMC
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa taasisi
    • Core Functions
  • Utawala
    • Idara
      • Human Resources and Administration
      • Health and Sanitation
      • Finance
      • Planning and Commercial
    • Vitengo
      • Maintenance Service
      • Internal Audit
      • Procurement Management
      • Information and Communication Technologies
      • Legal Services
      • Security
  • Kituo cha habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya picha
    • Press-Releases
    • Video
  • Marketing
    • Products and Services
    • Marketing Price
  • Investment and Projects
    • Ongoing Projects
    • Miradi iliyokamilika
    • Upcoming Projects
    • Fursa za Uwekezaji
  • Manunuzi
    • Tenders
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Journals/Newsletter
    • Reports
    • Hotuba
  • E- Services Links
    • Revenue Collection(TAUSI)
    • GISP Portal
    • Employees Self Service Portal
    • E - Mrejesho
    • E - Board
    • E - Mikutano

Mafunzo ya Afya kwa Watumishi Soko la Kariakoo

Posted on: May 10th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Mohamed Janabi, amewataka watumishi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo kujenga utamaduni wa kupima afya angalau mara moja kwa mwaka.

Alisema hatua hiyo itasaidia kutambua mapema dalili za magonjwa sugu yasiyoambukiza na hivyo kupata tiba kwa wakati, kuepusha athari zinazoweza kupunguza nguvu kazi ya taifa.

Prof. Janabi alitoa ushauri huo alipokuwa akizungumza wakati wa mafunzo ya siku moja kwa watumishi wa shirika hilo yaliyofanyika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ( Mei 9, 2025).

Katika mada yake kuhusu ugonjwa wa kiarusi, alieleza kuwa mtindo mbaya wa maisha, shinikizo la juu la damu, unywaji pombe kupita kiasi, na ulaji wa vyakula vyenye sukari na mafuta mengi ni sababu kuu zinazochangia ugonjwa huo.

"Ni muhimu kufanya uchunguzi wa afya zenu kila mwaka ili kuepuka kugundua magonjwa mkiwa katika hatua za mwisho au uzeeni, hali ambayo inaweza kusababisha madhara makubwa kwa afya zenu," alisisitiza Prof. Janabi ambaye ni mtaalamu bingwa wa magonjwa ya moyo.

 Prof.Janabi aliongeza kuwa dunia inakabiliwa na magonjwa mengi hatari kama vile moyo, shinikizo la damu, kisukari, figo, na kiarusi, ambayo yanasababisha vifo vingi. Hivyo, upimaji wa afya wa mapema ni muhimu ili kujua dalili na kupata matibabu stahiki.

Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, CPA. Ashraph Abdulkarim, alieleza kuwa shirika limeandaa mafunzo hayo kama sehemu ya mkakati wa kuwajengea uwezo watumishi wake ili waweze kufahamu hali zao za afya na kuchukua hatua za mapema kudhibiti magonjwa.

CPA Abdulkarim alishukuru Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa kutoa mafunzo kwa watumishi 35 ambao wana jukumu muhimu la kuhudumia wafanyabiashara na wananchi katika soko hilo.

Katika mada nyingine, Dkt. Garvin Kweka aliwaasa watumishi kuwa waaminifu kwa wenzi wao na kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya VVU/UKIMWI kwa kuepuka ngono zembe na matumizi mabaya ya vileo.

Naye Afisa Mwelimishaji kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Ilala, Bi. Mary Mwakyusa, aliwaonya watumishi dhidi ya vitendo vya rushwa wanapohudumia wafanyabiashara wa Soko la Kariakoo.

Matangazo

  • Taarifa kwa Umma January 31, 2025
  • Taarifa kwa Umma January 29, 2025
  • Usajili wa wafanyabiashara November 14, 2023
  • Tangazo la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 August 15, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Maandalizi Ufunguzi wa Soko la Kariakoo Yakamilika

    October 11, 2025
  • Meneja Mkuu Shirika la Masoko Kariakoo, Bw. Ashiraf Abdulkarim anasema Kariakooo ndiyo Soko kubwa ambalo wafanyabiashara wa ndani na nje ya mipaka ya Tanzania wanakuja kufanya biashara.

    September 24, 2025
  • Dkt. Jafo: Wafanyabiashara Kariakoo Kuweni Mabalozi wa Amani

    August 15, 2025
  • Soko la Kariakoo Kuwa na Bima ya Majanga

    July 31, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TAMISEMI
  • eGovernment Authority
  • Employees Self Service Portal

Viunganishi Linganifu

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    General Manager, Kariakoo Markets Corporation, Nyamwezi/Tandamti Street,

    Anuani ya posta: P. O. Box 15789 Dar es Salaam, Tanzania

    Simu: +255 22 2180678

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe za Watumishi: info@kariakoomarket.co.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

www.freevisitorcounters.com

    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2024 Shirika la Masoko ya Kariakoo . All rights reserved.