RAIS SAMIA AFUNGUA SOKO KUU LA KARIAKOO, ATAKA LIWE SOKO LA KUIGWA NDANI NA NJE YA NCHI.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema anataka Soko Kuu la Kimaitafa la Kariakoo liwe soko la mfano ambalo litaigwa na masoko mengine ya ndani na nje ya nchi kwakuwa na huduma zilipangiliwa vizuri kulingana na mahitaji ya soko na wadau wake.
Rais Samia amebainisha kuwa miongoni mwa mambo yatakalifanya soko hilo kuwa la mfano chini ni pamoja na uthabiti wa miundombinu ya kisasa ikiwemo mifumo ya Tehama, utaratibu mzuri wa maegesho, utaratibu mzuri kuingiza na kutoa mizigo sokoni, utaratibu kwa makundi mengine kuingia na kutoka sokoni ikiwemo boda boda, maguta n.k.
Rais Samia ameyasema hayo leo alipokuwa akiongea katika hafla ya ufunguzi wa Soko Kuu la Kariakoo lililokarabatiwa na kujengwa upya kwa gharama ya bilioni 28, fedha zilizotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita baada ya Soko hilo kupata ajali ya moto Julai 10, 2021.
Ameongeza kuwa uwekezaji uliofanywa na serikali ni mkubwa na umefanywa kupitia kodi za wananchi hivyo ni wajibu kila mwananchi kulinda miundombinu ya soko hilo na kuwataka wafanyabiashara kulipa kodi ya pango ili soko hilo liweze kujiendesha kwa manufaa ya sasa na baadaye.
Aidha, Rais Samia amueupongeza uongozi wa Shirika la Masoko Kariakoo kwa kujali makundi mbalimbali ya jamii ikiwemo kutenga chumba maalum kwa ajili ya wakina mama kunyonyeshea, kutoa ofisi kwa ajili ya huduma mbalimbali ikiwemo huduma za zimamaoto kwa lengo la kuimarisha za zimamoto kwa watu wa Kariakoo na maeneo ya Jirani.
Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, CPA. Ashraph Abdulkarim amemshukuru Mhe. Rais kwa kutoa fedha za ujenzi na ukarabati wa soko hilo, fedha ambazo zimewezesha kujenga soko jipya na hivyo kuongeza uwezo wa kuwahudumia wafanyabiashara ulinganisha na soko la awali kabla ya kuungua moto.
CPA. Abdulkarim ameongeza kuwa soko hilo litatoa huduma mbalimbali ikiwemo mauzo ya mizaa, mazao, huduma za kibenk, kubadilisha, migahawa, huduma za afya na huduma za maegesho ambayo yana uwezo wa kuegesha magari 400 kwa wakati mmoja hivyo kupunguza adha ya maegesho kwa eneo la Kariakoo.
Copyright ©2024 Shirika la Masoko ya Kariakoo . All rights reserved.