SHIRIKA LA MASOKO WAKUTANA NA OFISI YA MSAJILI WA HAZINA KWA TATHMINI YA UTENDAJI KAZI.
Uongozi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo umekutana na kufanya mazungumzo na wataalam kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina, wataalam hao wamekutana na Uongozi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo kwa lengo la kujitambulisha kabla ya kuanza kufanya zoezi la tathmini ya utendaji kazi wa shirika hilo kwa kipindi cha Julai, 2024 hadi Juni, 2025 na kipindi cha Julai 2025 hadi Desemba, 2025.
Akiongea katika kikao hicho, Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo CPA. Ashraph Abdulkarim amesema shirika hilo litatoa ushirikiano unaostahili ili wataalam hao waweze kufanya kazi yao kwa ufanisi na kupata matokeo stahii yatakayosaidia shirika hilo kusonga mbele zaidi.
“Ni desturi yetu kila inapofanyika tathmini au ukaguzi kila kinachohitajika kinapatikana kwa wakati, shirika hili ili liendelee kusonga mbele tumekubaliana menejiment yote kufanya kazi kwa ushirikiano na kuhakikisha hakuna kitu kinakwama, kutoa mrejesho kwa wadau wetu wa ndani na wakati wote” Ameongeza CPA. Abdulkarim
Kwa upande wake mkuu wa msafara kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina amebainisha kuwa tathmini itakayofanyika italisaidia shirika kubaini changamamoto, kutoa maoni yao kuhusu vigezo vya upimaji vilivyowekwa na hivyo kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.
Ofisi ya Msajili wa Hazina imeweka utaratibu wa kufanya tathmini ya utendaji kazi wa taasisi za umma zilizo chini ya usimamizi wake kila mwaka kwa lengo la kuimarisha utendaji kazi wa taasisi hizo ili zizalishe kwa tija na hatimaye ziweze kujiendesha zenyewe.
Copyright ©2024 Shirika la Masoko ya Kariakoo . All rights reserved.