• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Complaints |
    • Gms |
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

  • Mwanzo
  • About KMC
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa taasisi
    • Core Functions
  • Utawala
    • Idara
      • Human Resources and Administration
      • Health and Sanitation
      • Finance
      • Planning and Commercial
    • Vitengo
      • Maintenance Service
      • Internal Audit
      • Procurement Management
      • Information and Communication Technologies
      • Legal Services
      • Security
  • Kituo cha habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya picha
    • Press-Releases
    • Video
  • Marketing
    • Products and Services
    • Marketing Price
  • Investment and Projects
    • Ongoing Projects
    • Miradi iliyokamilika
    • Upcoming Projects
    • Fursa za Uwekezaji
  • Manunuzi
    • Tenders
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Journals/Newsletter
    • Reports
    • Hotuba
  • E- Services Links
    • Revenue Collection(TAUSI)
    • GISP Portal
    • Employees Self Service Portal
    • E - Mrejesho
    • E - Board
    • E - Mikutano

Shirika la Masoko ya Kariakoo kujiendesha kwa tija -CPA Ashraph

Posted on: April 4th, 2025

Watumishi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo wametakiwa kufanya mageuzi katika utendaji kazi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu, Miongozo na taaluma walizonazo ili kufikia malengo ya Taasisi na kuongeza tija.

Hayo yamesemwa na Meneja Mkuu wa Shirika hilo, CPA Ashraph Yusuph Abdulkarim wakati alipozungumza kwenye hafla fupi ya makabidhiano ya ofisi iliyofanyika leo (Aprili 4,2025) Dar es Salaam.

Meneja Mkuu huyo alisema endapo watumishi watafanya kazi kwa nidhamu na uadilifu ni dhahiri kwamba uzalishaji utaongezeka na mazingira ya kazi yataboreshwa na kuleta ufanisi mzuri katika utendaji kazi wa Shirika.

“Nitashirikiana na watumishi wenzangu kulifanya Shirika lisonge mbele na kujiendesha kwa tija pamoja na kudhibiti uvujaji wa mapato, kuongeza vyanzo vya mapato na kuweka mipango mizuri ya kibiashara” alisema CPA Ashraph.

CPA Ashraph amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kumuamini na kumteua kuongoza Shirika la Masoko ya Kariakoo kwa nafasi ya Meneja Mkuu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika hilo Hawa Ghasia, pamoja na kumkaribisha Meneja Mkuu huyo alimwagiza kusimamia kwa ukaribu mchakato wa maandalizi ya ufunguzi wa soko la Kariakoo uliopangwa ukamilike mwezi huu Aprili.

“Kazi yako kubwa kwa sasa ni kuhakikisha soko la Kariakoo linafunguliwa mwezi huu Aprili ili kuwezesha wafanyabiashara waweze kuingia ndani kuendelea na biashara kufuatia mradi wa ujenzi na ukarabati wa soko kukamilika,” alisema Ghasia.

Ghasia alisisitiza kuwa Bodi ya Wakurugenzi ina imani kubwa na Mtendaji Mkuu huyo kutokana na uzoefu alioupata alipokuwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili hivyo aweke mipango ya kujenga masoko mengine maeneo ya Shirika ya Mbezi Beach na Tabata Bima.

Naye Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Emma Lyimo aliyemwakilisha Katibu Mkuu kwenye hafla hiyo aliwasihi watumishi kutoa ushirikiano kwa Meneja Mkuu huyo ili atimize majukumu yake kwa ufasaha na kusaidia Shirika kufikia malengo ya kuanzishwa kwake.

Matangazo

  • Taarifa kwa Umma January 31, 2025
  • Taarifa kwa Umma January 29, 2025
  • Usajili wa wafanyabiashara November 14, 2023
  • Tangazo la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 August 15, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Maandalizi Ufunguzi wa Soko la Kariakoo Yakamilika

    October 11, 2025
  • Meneja Mkuu Shirika la Masoko Kariakoo, Bw. Ashiraf Abdulkarim anasema Kariakooo ndiyo Soko kubwa ambalo wafanyabiashara wa ndani na nje ya mipaka ya Tanzania wanakuja kufanya biashara.

    September 24, 2025
  • Dkt. Jafo: Wafanyabiashara Kariakoo Kuweni Mabalozi wa Amani

    August 15, 2025
  • Soko la Kariakoo Kuwa na Bima ya Majanga

    July 31, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TAMISEMI
  • eGovernment Authority
  • Employees Self Service Portal

Viunganishi Linganifu

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    General Manager, Kariakoo Markets Corporation, Nyamwezi/Tandamti Street,

    Anuani ya posta: P. O. Box 15789 Dar es Salaam, Tanzania

    Simu: +255 22 2180678

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe za Watumishi: info@kariakoomarket.co.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

www.freevisitorcounters.com

    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2024 Shirika la Masoko ya Kariakoo . All rights reserved.