• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Complaints |
    • Gms |
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

  • Mwanzo
  • About KMC
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa taasisi
    • Core Functions
  • Utawala
    • Idara
      • Human Resources and Administration
      • Health and Sanitation
      • Finance
      • Planning and Commercial
    • Vitengo
      • Maintenance Service
      • Internal Audit
      • Procurement Management
      • Information and Communication Technologies
      • Legal Services
      • Security
  • Kituo cha habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya picha
    • Press-Releases
    • Video
  • Marketing
    • Products and Services
    • Marketing Price
  • Investment and Projects
    • Ongoing Projects
    • Miradi iliyokamilika
    • Upcoming Projects
    • Fursa za Uwekezaji
  • Manunuzi
    • Tenders
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Journals/Newsletter
    • Reports
    • Hotuba
  • E- Services Links
    • Revenue Collection(TAUSI)
    • GISP Portal
    • Employees Self Service Portal
    • E - Mrejesho
    • E - Board
    • E - Mikutano

Wastaafu Soko la Kariakoo Kulipwa Milioni 306

Posted on: April 18th, 2025

Serikali ya Awamu ya Sita katika kuendelea kutatua kero za wafanyakazi nchini imefanikiwa kutoa shilingi Milioni Mia Tatu na Sita kwa ajili ya kulipa madeni ya waliokuwa watumishi wa Soko la Kariakoo.

Taarifa hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo Hawa Ghasia wakati wa kikao cha Kumi cha Bodi hiyo kilichofanyika ukumbi wa Arnautoglo Dar es Salaam jana Aprili 17,2025.

“Rais Samia Suluhu Hassan amesikia kilio cha waliokuwa wafanyakazi wa Shirika letu na kutupatia shilingi milioni 306 kulipa madeni. Nataka kuona ifikapo mwisho mwa wiki hii fedha zimelipwa kwa walengwa kwani wamesubiri kipindi kirefu” aliagiza Ghasia.

Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo CPA Ashraph Yusuph Abdulkarim alisema Shirika limepokea fedha hizo toka Hazina kufuatia maombi ya siku nyingi.

CPA Abdulkarim alibainisha kuwa fedha hizo zitalipwa kwa waliokuwa watumishi wa Shirika ambao kwa sasa wamestaafu ambapo umakini utazingatiwa ili haki itendeke.

Akitoa takwimu za wanaostahili kulipwa, Meneja wa Fedha wa Shirika la Masoko ya Kariakoo CPA Semeni Yamawe alisema jumla ya wastaafu kumi na tisa (19), pia wapo warithi ambao ndugu zao walikuwa watumishi lakini sasa ni marehemu pamoja na wastaafu ambao walishinda kesi mahakamani.

Katika hatua nyingine, Bodi ya Wakurugenzi imeelekeza Menejimenti ya Shirika kusimamia kikamilifu mpango kazi wa kuelekea ufunguzi wa soko la Kariakoo ikiwemo kuwapanga wafanyabiashara kwenye maeneo na kutoa mikataba ili shughuli zirejee sokoni.

Soko la Kariakoo linatarajia kurejesha shughuli zake hivi karibuni baada ya kukamilika kwa mradi wa kimkakati wa ujenzi wa soko jipya lenye sakafu nane na ukarabati wa lililokuwa soko kuu uliogharimu shilingi Bilioni 28.03 zilizotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita.

Mwisho.


Matangazo

  • Taarifa kwa Umma January 31, 2025
  • Taarifa kwa Umma January 29, 2025
  • Usajili wa wafanyabiashara November 14, 2023
  • Tangazo la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 August 15, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Maandalizi Ufunguzi wa Soko la Kariakoo Yakamilika

    October 11, 2025
  • Meneja Mkuu Shirika la Masoko Kariakoo, Bw. Ashiraf Abdulkarim anasema Kariakooo ndiyo Soko kubwa ambalo wafanyabiashara wa ndani na nje ya mipaka ya Tanzania wanakuja kufanya biashara.

    September 24, 2025
  • Dkt. Jafo: Wafanyabiashara Kariakoo Kuweni Mabalozi wa Amani

    August 15, 2025
  • Soko la Kariakoo Kuwa na Bima ya Majanga

    July 31, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TAMISEMI
  • eGovernment Authority
  • Employees Self Service Portal

Viunganishi Linganifu

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    General Manager, Kariakoo Markets Corporation, Nyamwezi/Tandamti Street,

    Anuani ya posta: P. O. Box 15789 Dar es Salaam, Tanzania

    Simu: +255 22 2180678

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe za Watumishi: info@kariakoomarket.co.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

www.freevisitorcounters.com

    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2024 Shirika la Masoko ya Kariakoo . All rights reserved.