• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Complaints |
    • Gms |
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
    • Majukumu ya msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Human Resources and Administration
      • Health and Sanitation
      • Finance
      • Planning and Commercial
    • Vitengo
      • Maintenance Service
      • Internal Audit
      • Procurement Management
      • Information and Communication Technologies
      • Legal Services
      • Security
  • Kituo cha habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya picha
    • Press-Releases
    • Video
  • Marketing
    • Products and Services
    • Marketing Price
  • Miradi na Fursa za uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Manunuzi
    • Zabuni
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Journals/Newsletter
    • Reports
    • Hotuba
  • Huduma mtandao
    • Revenue Collection(TAUSI)
    • GISP Portal
    • Employees Self Service Portal
    • E - Mrejesho
    • E - Board
    • E - Mikutano

WATUMISHI KARIAKOO WAPEWA MKONO WA SIKUKUU ZA MWISHO WA MWAKA, WAHIMIZWA KUENDELEA KUWAJIBIKA.

Posted on: December 22nd, 2025

WATUMISHI KARIAKOO WAPEWA MKONO WA SIKUKUU ZA MWISHO WA MWAKA, WAHIMIZWA KUENDELEA KUWAJIBIKA.


Shirika la Masoko ya Kariakoo limetoa zawadi za Sikukuu za Krismasi na mwaka mpya kwa watumishi wake ikiwa ni sehemu ya motisha kwa utendaji kazi wao mzuri waliouoneshakwa mwaka 2025 ambao umechangia shirika hilo kutoa huduma kwa wateja wake kwa ufanisi, weledi na kwa wakati.


Akikabidhi zawadi hizo, Meneja Mkuu wa Shirika hilo, CPA. Ashraph Abdulkarim amesema utendaji kazi wa watumishi wa shirika hilo umesaidia kuwapangia wafanyabishara wa zamani takribani 1520 maeneo ya biashara, kufanya uchambuzi na kuwapangia maeneo ya biashara wateja wapya 351, kuingiza mikataba ya wateja kwenye mfumo wa TAUSI na pia kushughulikia malalamiko na changamoto za wafanyabiasha kwa wakati na weledi.


Aidha, CPA. Abdulkarim amewahimiza watumishi hao kuendelea kufanya kazi kwa bidii, weledi na kufuata sheria, kanuni na taratibu zinazoongoza utumishi ili kuendelea kuchochea mabadiliko ya utendaji kazi wa shirika hilo na kutokubweteka.


CPA. Abdulkarim amebainisha kuwa soko la Kriakoo ambalo linasimamiwa na shirika hilo linapaswa kuendeshwa kisasa na kulifanya liwe soko linalotoa huduma anuai badala ya kuwa soko la mazao ya kilimo pekee kama ilikuwa hapo awali.


“Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inataka kuona matokeo, hivyo kila mmoja katika nafasi yake anapaswa kuona ni kwa namna gani anaweza kuleta matokeo chanya katika kutoa huduma na kufanya shirika hilo kujiendesha kibiashara zaidi” ameongeza CPA. Abdulkarim


CPA. Abdulkarim ameongeza kuwa ili kuhakikisha watumishi wanafanya kazi vizuri, shirika litaendelea kusimamia na kutoa stahiki zao kwa wakati, huku ikiweka mkazo katika kuwajengea uwezo wa mara kwa mara ili kuendana na mabadiliko yanayojitokeza mara kwa mara duniani.


Matangazo

  • Taarifa kwa Umma January 31, 2025
  • Taarifa kwa Umma January 29, 2025
  • Usajili wa wafanyabiashara November 14, 2023
  • Tangazo la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 August 15, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI KARIAKOO WAPEWA MKONO WA SIKUKUU ZA MWISHO WA MWAKA, WAHIMIZWA KUENDELEA KUWAJIBIKA.

    December 22, 2025
  • SOKO LA KARIAKOO MBIONI KUFUNGULIWA

    December 19, 2025
  • SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO LAANZA KUANDAA MPANGO MKAKATI WA MIAKA MITANO 2026-2031.

    December 12, 2025
  • ASKARI WA SHIRIKA LA MASOKO KARIAKOO WANOLEWA KUHUSU HUDUDUMA BORA KWA MTEJA.

    December 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TAMISEMI
  • eGovernment Authority
  • Employees Self Service Portal

Viunganishi Linganifu

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    General Manager, Kariakoo Markets Corporation, Nyamwezi/Tandamti Street,

    Anuani ya posta: P. O. Box 15789 Dar es Salaam, Tanzania

    Simu: +255 22 2180678

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe za Watumishi: info@kariakoomarket.co.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

www.freevisitorcounters.com

    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2024 Shirika la Masoko ya Kariakoo . All rights reserved.