Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, CPA Ashraph Abdulkarim, amewataka watumishi wa Shirika hilo kufanya kazi kwa bidii na kuepuka mazoea yanayopunguza tija, ikiwemo kutoheshimu muda na kutotekeleza maelekezo ya viongozi.
Akizungumza leo Juni 27, 2025 jijini Dar es Salaam katika hafla ya kumuaga mtumishi mstaafu Flavian Mlelwa, CPA Abdulkarim amesisitiza kujifunza kutoka kwa Mlelwa ambaye ametumikia Shirika kwa miaka 37 kwa bidii, uvumilivu na uzalendo.
Kwa upande wake, Mlelwa aliyestaafu Machi 2025 alisema alianza kazi mwaka 1988 na kupitia changamoto na mafanikio, akitaja tukio la moto wa Soko Julai 10, 2021 kama baya zaidi.
Mlelwa ameishukuru Serikali kupitia Shirika la Masoko ya Kariakoo kwa kumpatia stahiki zote za kustaafu, ikiwemo nauli ya kurejea nyumbani Makete na malipo ya mkono wa kwaheri kwa mujibu wa mkataba wa hali bora.
General Manager, Kariakoo Markets Corporation, Nyamwezi/Tandamti Street,
Postal Address: P. O. Box 15789 Dar es Salaam, Tanzania
Telephone: +255 22 2180678
Mobile:
Email: info@kariakoomarket.co.tz
Copyright ©2024 Shirika la Masoko ya Kariakoo . All rights reserved.